Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

"Natumia ubabe kupata Suluhu" DC Sabaya akihojiwa Clouds360

Screenshot 2021 05 10 At 10.58.25 660x400.png "Natumia ubabe kupata Suluhu" DC Sabaya akihojiwa Clouds360

Mon, 10 May 2021 Chanzo: millardayo.com

“Lengai_ole_sabaya ni mtu anayechanyanga njia zote ili kupatika suluhu ya haki za wananchi ambaye anaweza kuwa Mbabe kama kuna ubabe, anaweza kuwa mpole pia ni mtu wa imani na kusali kama Suluhu itapatikana kwa njia hiyo. Natumia njia zote hizo ili kupata suluhu na majawabu ya wanachi” DC Sabaya

“Mimi ni mtu wa kawaida tu ambaye anatoka kwenye background ya kawaida kabisa ya maisha ya kawaida kabisa. Nahangaika na watu na cha kwanza ni kuwasaidia watu wa kawaida kabisa ili wapate haki zao, inawezekana njia hizo zikawa na tafsiri nyingi hasa kwenye majukumu ya Mkuu wa wilaya” DC Sabaya

“Huwezi kumfurahisha kila mtu kupata Suluhu ya wananchi na majawabu ya kero za watu, mwingine ukimwambia acha anaacha, kuna mwingine ukimwita ukimwambia sijapenda anakoma, mwingine ukimfokea anaacha na mwingine ukimkamata ndio anaacha kwahiyo kama kwahiyo hizi njia zote zinatumika ili nipate. Kwahiyo ukiwa Kiongozi unatumia njia tofauti tofauti kulingana na Mazingira husika” Mkuu wa wilaya ya Hai

LIVE: KIMEUMANA SIMBA VS YANGA, ‘MBWAI MBWAI’ IMEAHIRISHWA

Chanzo: millardayo.com