Sun, 4 Jul 2021
Chanzo: www.habarileo.co.tz
MENEJA wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC) Mkoa wa Mara, Eliaisa Keenja amepongeza wapangaji wa majengo mkoani humo kwa jinsi wanavyolipa kodi za pango vizuri.
Keenja amesema tofauti na hali ilivyo kwingine, mkoani Mara wapangaji wengi wanalipa kodi kwa wakati na ambao wanashindwa kufanya hivyo kutokana na sababu zilizo nje ya uwezo wao wamekuwa wakipeleka taarifa kwa maandishi.
Kwa mujibu wa Keenja, wapangaji ambao hawatimizi wajibu wao huo ni wachache sana.
Chanzo: www.habarileo.co.tz