Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mzee aliyekimbiwa na mke kisa maskini, ajenga ghorofa la mil 300

Jumanne Kingu B.jpeg Mzee aliyekimbiwa na mke kisa maskini, ajenga ghorofa la mil 300

Wed, 1 Mar 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mzee Jumanne Kingu kutoka Mkonoo jijini Arusha, Tanzania sasa anajenga nyumba yake ya kifahari yenye thamani ya Tsh milioni 300 ikiwa ni miaka kadhaa baada ya mkewe kumkimbia kwa sababu ya kuwa maskini hohehahe.

Kingu amesema alikuwa akiishi katika nyumba ya mabanzi na alikuwa maskini wa kutupwa, hana mbele wala nyuma kiasi kwamba kitandani kwake alikuwa ametandika suruali zilizoisha hata hakuwa na blanketi ya kujifunika hali iliyomfanya mkewe kutoroka.



"Nilikuwa nikivaa suruali zilizochanikachanika. Nilikuwa nikilala kitandani kwangu nilikuwa nimetandika suruali zilizoisha ndiyo nimetandika kitandani. Hata nguo za kujifunika sina. Lakini sikukata tamaa na maisha," amesema mzee Kingu.

“Baadaye nilipata hela nikajenga hii nyumba ya mbao na kufanya kazi, nikahamia kwa hii nyumba ya mbao kisha nilikuwa nikipata hela nanunua ng’ombe, nikipata hela nanunua mbuzi, nikawa nafuga,” aliongeza.

Akiwa na mifugo hiyo, Kingu alianza kuwauza na kununua ardhi ambayo aliigawanya na kuwauzia wanunuzi wengine. Hivi ndivyo alianza biashara yake ya mali isiyohamishika.

"Ninaziuza mwenyewe; nachukia madalali kwa sababu wanamuuzia mtu mmoja kisha kumuuzia mwingine," alifafanua.

Kingu ni mzee ambaye hivi karibuni aliachiwa huru baada ya kukabiliwa na tuhuma za kuwanyanyasa kijinsia watoto 22 lakini kesi hiyo ilifutwa. Sasa anasema kuwa kesi hiyo ilichochewa na watu waliokuwa wakimuonea wivu kwa sababu ya mafanikio yake ambayo ni pamoja na kujenga nyumba yake ya Tsh milioni 300.

“Walionifanyia haya ni walimu, wamesoma, wana vyeti na wanapata mikopo na mimi sina,” alisema. Mzee huyo mwenye ari pia anamiliki kinu cha kwenda chini na mashine ya kusaga inayowahudumia wanakijiji.

Lakini sasa wanakijiji wanasema yeye ni Freemason, ambaye amefuga nyoka na mwanamke mwenye titi moja. Majirani wengine nao wanadai kuwa kuna Mwarabu anayeishi Oman ambaye ndiye mmiliki wa nyumba hiyo huku wengine wakisema kuwa utajiri wake ni wa mwanamke tajiri mwenye gari kubwa.

“Nilipokuwa maskini walikuwa wakiniita mchawi lakini sasa hivi ni tajiri wanasema mimi ni Freemason, nina nyoka na mwanamke ndani ya nyumba,” alisema. Nyumba ya kifahari ya Kingu ni ya ghorofa tatu na kila chumba kina bafu lake lenye mfumo wa maji moto na baridi.

Nyumba hiyo ina vyumba vinne kwenye ghorofa ya chini, vyumba viwili na chumba cha kupumzika kwenye ghorofa ya kwanza na ghorofa ya pili ina chumba na mahali pa kupumzikia kupunga hewa safi.

Wanamtandao Japo mzee huyo anatafuta mke, bado ana hofu ya kuachwa na mke wa kwanza. "Ninamwomba Mungu anipe mke mwema. Ninahitaji mke, hata leo niko tayari kuoa," alisema.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live