Hatimaye mwili wa mwisho ya miili 13 iliyokuwa ikitafutwa kwa muda wa siku nne sasa baada ya kuzama ndani ya ziwa Victoria umepatikana na kuhitimisha kazi hiyo ya kutafuta miili hiyo.
Mwili huo umepatikana leo Jumatano Agosti 2,2023 saa 7 mchana baada ya miili mingine kuopolewa kuanzia jana Agosti Mosi saa 7 mchana hadi leo asubuhi.
Julai 30,2023 saa 12.30 jioni mitumbwi miwili iliyokuwa imebeba waumini 28 wa Kanisa Takatifu la Mungu wa Kiroho (KTMK) ilizama ziwani ambapo watu 14 waliokolewa na kukimbizwa hospitalini.
Katika tukio hilo ambapo wengi walikuwa ni watoto na wanafunzi wa Shule ya Msingi Bulomba wilayani Bunda, watu 13 walizama ambapo shughuli ya kuwatafuta ilianza kesho yake.