Pangani. Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Pangani, Hamis Mnegero (72), amefariki dunia akiswali swala ya alfajiri leo Alhamisi Mei 9, 2019.
Katibu wa CCM Mkoa wa Tanga, Shaibu Akwilombe, amesema Mngero alipatwa na mauti katika msikiti mkuu wa Ijumaa uliopo katika kijiji cha Sakura wilayani humo.
Mkunde Hamis, mtoto wa marehemu amesema wakati akielekea msikitini baba yake hakuwa na tatizo lolote.
“Jana tumefuturu naye akiwa na afya njema akaenda kuswali na kurejea salama na leo aliamka na kwenda msikiti mkuu wa Ijumaa kuswali akiwa haumwi chochote,” amesema Mkunde.
Mnegero amekuwa mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Pangani kwa miaka 25.