Bunda. Miradi 62 yenye thamani ya zaidi ya Sh31.1 bilioni inatarajiwa kuzinduliwa, kukaguliwa na kuwekewa mawe ya msingi mkoani Mara katika mbio za mwenge wa uhuru.
Miradi hiyo ni ya sekta ya elimu, maji, kilimo, afya, utalii, ujenzi, ustawi wa jamii, viwanda na biashara na ajira itatembelewa na mbio hizo katika halmashauri tisa za mkoa wa Mara kuanzia leo Jumanne Mei 28, 2019.
Akizungumza katika kijiji cha Serengeti wilayani Bunda leo wakati akipokea Mwenge huo kutoka Mkoa wa Simiyu, mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima amesema katika mbio hizo kutakuwa na kumbukumbu maalumu ya Julius Nyerere.
“Mbali na kuwasha Mwenge wa Mwitongo kijijini Butiama, pia tunatarajia kufanya kumbukumbu ya Nyerere, muasisi wa mwenge wa uhuru nchini,” amesema Malima.
Katika makabidhiano hayo mkuu wa Mkoa wa Simiyu,
Anthony Mtaka amesema mkoani kwake mwenge huo umezindua miradi 34 yenye yenye thamani ya Sh8.5 bilioni.
Pia Soma
- Upande wa utetezi kesi ya Kisena na wenzake wahoji upelelezi kutokamilika
- Mashtaka matatu anayedaiwa kumteka Mo Dewji haya hapa
- Mutharika ashinda urais Malawi
- Wasichana wapewe elimu ya kuwashinda wakware