Fri, 3 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mwanasheria wa Halmashauri ya Wilaya ya Iringa, Stellah Makali amefariki dunia baada ya gari aliyokuwa akisafiria kugongana na lori.
Ajali hiyo imetokea jana Novemba 02, 2023 katika eneo la Ihemi kata ya Mgama mkoani Iringa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Allan Bukumbi amesema ajali hiyo imehusisaha gari dogo aina ya Noah na lori la mizigo.
Bukumbi amesema lori hilo lilihama njia kisha kugongangana na Noah uso kwa uso na kusababisha kifo cha Stellah aliyefariki papo hapo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live