Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwananchi yaiibua halmashauri Buchosa, yaahidi kujenga choo cha shule

Mwananchi yaiibua halmashauri Buchosa, yaahidi kujenga choo cha shule

Sat, 26 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Buchosa. Siku moja baada ya Mwananchi kuandika habari ya walimu na wanafunzi Shule ya Sekondari Bukokwa wilayani Sengerema kutumia choo kimoja, halmashauri hiyo imeahidi kumalizia ujenzi wa choo hicho kilichoanza kujengwa na wananchi.

Akizungumza leo Jumamosi Oktoba 26, 2019

ofisa elimu Sekondari Halmashauri ya Buchosa, Bruno Sangwa amesema baada ya kupata taarifa hiyo alifika katika shule hiyo na kujionea hali halisi.

Amesema kutokana na kushuhudia wanafunzi na walimu wanavyopata shida, wameamua kumalizia ujenzi huo.

"Nimejionea hali halisi, halmashauri tumeamua kumalizia ujenzi wa choo hiki,” amesema.

Mwenyekiti wa kijiji cha Bukokwa, Peles Nzobana ameipongeza halmashauri hiyo kumalizia ujenzi huo, sasa walimu hawatatumia choo kimoja na wanafunzi.

Pia Soma

Advertisement
Mkazi wa kijiji hicho, Juma Kanazi amesema ushirikiano katika kila jambo ni kitu muhimu huku akiipongeza Mwananchi kwa kuripoti jambo hilo.

Shule hiyo ina wanafunzi 220 na walimu 11 huku ikikabiliwa na upungufu wa vyumba 12 vya madarasa.

 

Chanzo: mwananchi.co.tz