Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mwanamke aliyeuawa kwenye mkanyagano Tanzania alikuwa anamuenzi Rais Magufuli

Ae9a5e853a1034b9 Mwanamke aliyeuawa kwenye mkanyagano Tanzania alikuwa anamuenzi Rais Magufuli

Wed, 24 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Susan Mtuwa alifariki dunia Jumapili, Machi 21 pamoja na wanawe wanne kutokana na mkanyagano walipokuwa wamekwenda kuutizima mwili wa Hayati Magufuli

- Familia ya Susan imesema kwamba mama huyo alimpenda na kumuenzi sana Rais Magufuli na ndio sababu aliamua kuhudhuria ibada ya wafu kwa mwendazake

- Susan alikuwa ameambia watu kadhaa wa familia yake kwamba angefika katika uwanja wa Uhuru ili kumuaga mpendwa Rais Magufuli

Mama aliyepoteza maisha yake pamoja na wanawe wanne katika mkanyagano uwanjani Uhuru akiutizama mwili wa Hayati Magufuli anasemekana alikuwa mfuasi wake sugu.

Susan Mtuwa aliaga dunia Jumapili, Machi 21 aking'ang'ana kuutizama mwili wa mwendazake Rais John Pombe Magufuli.

Kulingana na familia yake,Susan alimpenda sana Magufuli na hata alikuwa amewahimiza baadhi ya jamaa wake waandamane naye kumuaga marehemu.

Mmoja wa familia yake akizungumza na vyombo vya habari alisema kwamba Susan alikuwa anaongopa kutangamana na umati mkubwa tangu mlipuko wa virusi vya COVID- 19 uliripotiwa lakini alisema hangekosa kumuaga Magufuli kwa ajili ya hilo.

" Susan alimpenda sana Magufuli lakini singelijua kwamba angeenda kuhudhuria hafla hiyo kwa sababu alikuwa anaogopa sana umati mkubwa kwa ajili ya ugonjwa wa corona," Mamake aliyetambulika kama Illuminata alisema.

Kama ilivyoripotiwa awali na TUKO.co.ke, Susan aliondoka nyumbani kwake mwendo wa saa kumi na mbili asubuhi kwenda uwanja wa Uhuru kumuaga hayati Magufuli.

" Tulimpigia simu jioni lakini hakupokea, muda mchache baadaye mtu tusiyemjua akapiga, akatueleza kwamba Susan alikuwa amehusika kwenye mkanyagano," George Mtuwa ambaye ni jamaa wake aliambia vyombo vya habari.

George alisema aliandamana na baadhi ya jamaa wake hadi katika uwanja huo ili kubaini kile kilichokuwa kimetendeka, waliwatafuta katika hospitali kadhaa lakini hawakuwapata ila kupata miili yao baadaye kwenye mochuari.

Susan anasemekana kuondoka nyumbani na mjakazi wake na kufikia sasa hajulikani aliko, shughuli za kumtafuta zimeanzishwa.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke