Mwanamke mmoja Mkazi wa Kijiji cha Kanyarakata Kata ya Mbuluma Wilayani Kalambo Mkoani Rukwa, Albetina Mazwile (42) amefariki baada ya kupigwa fimbo katika sehemu mbalimbali za mwili wake na Mumewe na kupelekea kuvuja damu kwa ndani.
Mwanamke mmoja Mkazi wa Kijiji cha Kanyarakata Kata ya Mbuluma Wilayani Kalambo Mkoani Rukwa, Albetina Mazwile (42) amefariki baada ya kupigwa fimbo katika sehemu mbalimbali za mwili wake na Mumewe na kupelekea kuvuja damu kwa ndani. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, William Mwampaghale amesema chanzo cha Mume kumpiga Mkewe ni chuki binafsi "Tunamshikilia Mwanaume huyu tukikamilisha uchunguzi tutamfikisha Mahakamani"