Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mvua yaharibu miundombinu ya shule nne mkoani Lindi

Mvua yaharibu miundombinu ya shule nne mkoani Lindi

Mon, 17 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Kilwa. Mvua zinazoendelea kunyesha wilayani Kilwa Mkoa wa Lindi zimeharibu miundombinu ya shule za msingi Njinjo, Kisima Mkika, Ndende, Ruhatwe pamoja na kituo cha afya Njinjo.

Akizungumza leo Jumamosi Februari 15, 2020 mkurugenzi wa halmashauri ya Kilwa, Jofrey Jafari amesema kijiji cha Njinjo kimeathirika zaidi na mafuriko, wananchi wote wamehamishiwa kijiji cha Kipindimbi.

Amebainisha kuwa wanafunzi waliokuwa wakisoma katika shule  ya Njinjo wameamishiwa katika shule nyingine zilizopo jirani.

"Shule ya msingi Njinjo tumeifunga kabisa na wanafunzi wote wamehamishwa. Halmashauri inaendelea kufanya marekebisho ya  miundombinu iliyoharibiwa na mafuriko  hayo lakini shule. Tutatoa eneo jingine kwa ajili ya kujenga shule mpya,” amesema.

Amesema mvua hiyo imesababisha vyoo vya shule ya msingi, sekondari na zahanati kuharibika.

Amebainisha kuwa wananchi waliokumbwa na mafuriko wapo katika maeneo waliyopewa na Serikali kwa ajili ya kuanzisha makazi mapya na yale ya awali kuwa mashamba.

Pia Soma

Advertisement

Chanzo: mwananchi.co.tz