Tue, 9 Apr 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mvua kubwa iliyoambatana na upepo, imebomoa nyumba 17 huku nyingine 61 zikiezuliwa mapaa katika Kijiji cha Lyasembe, Kata ya Murangi, jimbo la Musoma Vijijini mkoani Mara.
Mvua kubwa iliyoambatana na upepo, imebomoa nyumba 17 huku nyingine 61 zikiezuliwa mapaa katika Kijiji cha Lyasembe, Kata ya Murangi, jimbo la Musoma Vijijini mkoani Mara. Tukio hilo lilitokea Machi 5 mwaka huu, huku watu 685 wakiathirika wakiwamo watoto 384 na watu wazima 301, lakini pia vyumba viwili vya madarasa ya Shule ya Msingi Lyaembe vikibomoka.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live