Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mvua kubwa kunyesha Dar

Tue, 25 Sep 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetahadharisha kutokea mvua kubwa ndani ya siku tatu kuanzia kesho hadi Alhamisi Septemba 27, 2018,.

Kutokana na utabiri huo, TMA imewataka wananchi kuchukua tahadhari.

Taarifa ya mamlaka hiyo, iliyotolewa leo jioni Septemba 25,2018 imetaja mikoa itakayoathirika na mvua hizo ni Tanga, Dar es Salaam, Pwani pamoja na Visiwa vya Pemba na Unguja.

Taarifa hiyo imewataka wananchi wa maeneo husika kuchukua tahadhari kwa sababu mvua hizo ni kubwa kwa zaidi ya asilimia 70.

“Madhara yatakayotokana na mvua hiyo ni kutokea mafuriko katika mitaa na kusababisha msongamano wa magari na watu hivyo kuchelewesha usafirishaji hasa katika maeneo ya mjini,” imesema taarifa hiyo ya TMA

 

Chanzo: mwananchi.co.tz