Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mvua Dar yavuruga soko la ‘mahakama ya ndizi’

Mvua Dar yavuruga soko la ‘mahakama ya ndizi’

Thu, 6 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Mvua inayonyesha katika vipindi tofauti jijini Dar es Salaam imesababisha miundombinu ya soko la Mabibo maarufu ‘mahakama ya ndizi’ kuharibika na kusababisha usumbufu kwa wafanyabiashara na wanaofika sokoni hapo kununua bidhaa mbalimbali.

Kuanzia katika lango kuu la kuingilia soko hilo kuna matope hadi zilipopangwa bidhaa zinazouzwa kwa wateja.

Changamoto hiyo imekuwa fursa kwa baadhi ya vijana walioanzisha biashara ya kukodisha buti za mvua kwa wanaoingia kununua bidhaa.

Ukifika getini haraka vijana hao wanakuchangamkia na kukupatia buti hizo zinazokodishwa kwa Sh1,000.

Ukichana na ukodishaji wa buti huduma ya kuoshwa miguu inatolewa pia kwa wale ambao hawawezi kukodi viatu.

Elina Kingu ni mmoja wa watu waliokodi buti hizo baada ya kuona kwa viatu vyake asingeweza kukanyaga tope hilo.

Pia Soma

Advertisement
“Mwanzoni nilikuwa mbishi ila kadiri nilivyosogea nikaona hakuna namna naweza kukanyaga haya matope, nimelazimika kulipa elfu moja nipate hizo buti ingawa kiukweli sikuwa na bajeti hiyo,” amesema Kingu.

Meneja wa soko hilo Moses Olomi amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo na kueleza kuwa inatokana na asili ya eneo husika.

“Hapa tumeshaweka vifusi hadi basi, ni eneo lenye asili ya maji hivyo mvua zinaponyesha hali hii ni ya kawaida na hata wafanyabiashara wenyewe wameshazoea huwa wanajiandaa,” amesema Olomi.

Chanzo: mwananchi.co.tz