Mon, 27 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Katibu Tawala Wilaya ya Mvomero, Said Nguya amesema wanajivunia wilaya hiyo kuwa kitovu cha elimu nchini hivyo watu wanapaswa kufahamu mchango wao katika elimu.
Ameyasema hayo wakati akitoa salam za Serikali ya Wilaya ya Mvomero katika Convocation Chuo Kikuu Mzumbe, mbele ya Waziri wa Elimu, Prof Adolf Mkenda na Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Adam Malima.
Alitumia fursa hiyo kutoa msisitizo katika masuala kadhaa moja ni kupigia mstari mkubwa watu wafahamu kuwa Chuo Kikuu Mzumbe kipo Wilaya ya Mvomero na sifa zote za Chuo hicho Serikali ya Wilaya na Mkoa ina mchango wake. -
Chanzo: www.tanzaniaweb.live