Mkuu wa wilaya na Arumeru Jerry Muro amekabidhi kiasi cha 6,400,000 kwa wananchi ambao Ng’ombe zao 16 ziliuwawa katika hifadhi ya taifa ya Arusha (Arusha national park)
Hatua hiyo ya DC Muro imekuja kufuata kilio cha wananchi ambao Ng’ombe zao ziliuwawa kwa kuingia hifadhi na kisha kuanza kuleta uharibifu wa wanyama na hifadhi kutokana na Ng’ombe hao kupata kichaa wakiwa juu ya Hifadhi na kusababisha askari wa hifadhi kuwaua
Hata hivyo DC Muro amewaonya wananchi kuacha kulisha mifungo yao karibu na eneo la hifadhi, kwani mifungo kuingia katika maeneo ya hifadhi ni kinyume cha sheria.
Kwa upande wao Baadhi ya Wananchi wamemshukuru DC Muro na wadau wote waliousika kwa namna yeyote kwa kuwapatia kifuta machozi hicho.