Mwajuma Mwiru, Mkazi wa Negamsi, Wilaya ya Babati, mkoani Manyara, ameziomba mamlaka za serikali, kulisukuma Jeshi la Polisi mkoani humo, kupeleka mahakamani kesi ya mwanae kunajisiwa na na mtu anayedaiwa kuwa mfanyakazi wa Shirika la Compasion Intenational.
Mtoto huyo (jina limehifadhiwa), anadaiwa kunajisiwa na mfanyakazi wa shirika hilo, baada ya kumrubuni kwa kumtuma amuingizie kopo la sabuni chumbani kwake, na kisha kuwasha redio kwa sauti ya juu na kuanza kutekeleza ukatili huo.
Mwajuma, ambaye ni mama mzazi wa mtoto huyo, amesema kesi hiyo imeshindwa kupekelekwa mahakamani kwa miezi saba sasa.