Mtoto Yusuph Salum (9) mkazi wa Rutamba Manispaa ya Lindi, ambaye alichomwa moto na mvuke wa maji na mganga wa kienyeji kwa dhamira ya kumtibu ugonjwa wa degedege, amefariki dunia katika Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Lindi Sokoine wakati akipatiwa matibabu ya vidonda hivyo.
Inasemekana kwamba, mama mzazi wa mtoto Yusuph ambaye ni mkazi wa Rutamba, alimpeleka mwanaye nyumbani kwa mganga wa kienyeji aliyefahamika kwa jina la Jalina Juma Jiwalila, mwenye umri wa takriban miaka 40 kwa lengo la kupatiwa matibabu ya ugonjwa wa Degedege uliokuwa unamsumbua
Baada ya kumfikisha mganga huyo aliahidi kumtibu na ndipo alipomlaza chali kwenye kitanda ambacho hakikuwa na godoro na kisha chini aliweka nyasi na kuziwasha moto uliopelekea kumuunguza sehemu za mgongoni na kumsababishia majeraha makubwa.