Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Msando: Puuzieni uzushi kuhusu Msomera

MSANDOO 3 660x400 Msando: Puuzieni uzushi kuhusu Msomera

Thu, 14 Sep 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mkuu wa wilaya ya Handeni, Albert Msando amesema wakazi wa Kijiji cha Msomera hawana tatizo lolote na serikali wala wizara ya mifugo na uvuvi, hivyo kuiomba jamii kupuuza yanayosemwa na baadhi ya watu wasioitakia mema serikali katika utekelezaji wa majukumu yake.

Msando ametoa kauli hiyo mbele ya Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega aliyefika kijijini hapo kuzungumza na wakazi wa Msomera.

Amesema kijiji cha Msomera ni kijiji kilichopangwa kwa kufuata mpango wa matumizi bora ya ardhi ikiwa ni pamoja na kutenga maeneo ya malisho na josho kwa ajili ya mifugo.

Katika awamu ya kwanza mpaka sasa tayari kaya 500 zimeshaanza makazi mapya kijijini Msomera zikitokea Hifadhi ya Taifa ya Ngorongoro na awamu ya pili ya kuwapokea wengine inatarajia kuanza Septemba 25 mwaka huu.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live