Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Msalagambo' kumaliza tatizo la miundombinu Handeni

60033 PIC+MSALAGAMBO

Tue, 28 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Handeni. Katika kumaliza changamoto ya uhaba wa miundombinu shuleni, Wilaya ya Handeni imeanzisha mtindo wa 'Msalagambo' wa kuwajumuisha wazazi na walezi kushiriki kwenye shughuli za ujenzi wa madarasa.

Kupitia Msalagambo, kila Jumamosi wananchi hukutana kushiriki ujenzi wa madarasa kwenye shule za vijiji vyao ili kumaliza uhaba uliopo.

Akizungumza kwenye wiki ya elimu inayoendelea wilayani kwa ufadhili wa Mtandao wa Elimu Tanzania (Tenmet) leo Jumatatu Mei 27,2019, Mkuu wa Wilaya ya Handeni, Godwin Gondwe amesema walikuwa wanakabiliwa na uhaba wa madarasa 62.

“Kupitia 'Msalagambo' ujenzi wa madarasa haya umefikia asilimia 90 kwa sababu wananchi wakijitolea, Serikali inaongezea nguvu, kwenye kila Msalagambo  sisi viongozi hatukosekani,” amesema Gondwe.

 

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Martine Shigella amesema mkakati uliopo mkoani humo ni kuhakikisha wanaongeza ufaulu na kuondoa sifuri.

Pia Soma

“Uchumi wa viwanda unawategemea wasomi na wasomi hawa watapatikana tukiandaa mazingira mazuri ya elimu, ukilinganisha na zamani, mkoa huu umepiga hatua,” amesema Gondwe.

Amesema wamekamilisha ujenzi wa vyumba vya maabara na kwamba katika bajeti ya mwaka 2018/2019 na 2019/2020 kipaumbele ni vifaa kwa ajili ya maabara hizo.

Awali, Mwakilishi wa Mratibu wa Tenmet, Clement Mganga amesema sababu ya kuchagua wilaya ya Handeni ni mfululizo mzuri wa matokeo mazuri ya darasa la saba na sekondari wanayoyapata mwaka hadi mwaka.

Ufaulu wa darasa la saba Handeni Vijijini umepanda kutoka asilimia 73.5 mwaka 2017 hadi 81.6  mwaka 2018 wakati Handeni mjini ni asilimia 78 hadi asilimia 80 mwaka jana.

Chanzo: mwananchi.co.tz