Katavi. Zaidi ya vibanda vitano vya soko kuu mjini Mpanda Mkoani Katavi, Tanzania, vimeteketea kwa moto ulioanza ghafla usiku wa kuamkia leo.
Shuhuda wa tukio hilo, Ayoub Kassim amesema moto huo ulianza ghafla saa sita usiku na kuteketeza mali za wafanyabiashara zilizokuwemo kwenye vibanda hivyo.
“Moto huo umesababishwa na hitilafu ya umeme,” amesema Kassim.
Hata hivyo, Jeshi la Zimamoto Mkoa wa Katavi limewahi kufika eneo la tukio na kufanikiwa kuudhibiti moto huo uliokuwa ukisambaa kwa kasi.
Hadi sasa bado haijafahamika thamani ya mali zilizoteketea katika tukio hilo.
Endelea kufuatilia Mwananchi kwa taarifa zaidi kuhusu tukio hili.