Fri, 6 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Moto mkubwa ambao bado chanzo chake hakijajulikana umeteketeza Bar ya A Square iliyopo Ubungo Kibangu Jijini Dar es salaam usiku huu na kusababisha hasara kwa Wamiliki wa Bar hiyo.
Mashuhuda na mmiliki wa Bar hiyo wamesema hawajui chanzo cha moto huo kwasababu hakukuwa na ishara yoyote na shughuli zilikuwa zikiendelea kama kawaida.
“Kilichotushangaza moto umeanzia juu ya paa tena tumefanya kuambiwa maana hapa shughuli zilikuwa zikiendelea kama kawaida, tukasikia kelele kwamba moto unawaka juu na kwa vile Bar imeezekwa kwa makuti ikawa rahisi kushika moto kwa haraka”
Chanzo: www.tanzaniaweb.live