Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mnyeti atoa neno kushuka mapato ya Tanzanite

11946 Pic+mnyeti TanzaniaWeb

Mon, 23 Jul 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Mirerani. Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti amesema hakuna utoroshaji wa madini ya Tanzanite uliofanyika hadi kusababisha kushuka kwa malipo ya mrabaha kutoka Sh444 milioni hadi Sh40 milioni kwa mwezi.

Amesema hali hiyo inatokana na uzalishaji mdogo wa madini hayo migodini na kusababisha mapato kushuka.

Mnyeti amesema hayo leo Julai 22, 2018 wakati akizungumzia na Mwananchi kuhusu  taarifa iliyotolewa hivi karibuni kuwa mapato ya mrabaha kwa sababu ya utoroshaji.

Amesema mapato hayajashuka sababu ya madini kutoroshwa ila mapato yameshuka baada ya uzalishaji kuwa duni kwenye kipindi cha miezi mitatu iliyopita katika migodi ya madini ya Tanzanite.

"Kuanzia Aprili, Mei na Juni hakukuwa na uzalishaji mkubwa ila ilikuwa ni kwenye mgodi mmoja wa kampuni ya Iraqw mining ndiyo ulizalisha kwa kiasi kikubwa zaidi ya migodi yote," amesema Mnyeti.

Amesema mrabaha ungepatikana mkubwa kutokana na migodi hiyo kuzalisha madini mengi lakini siyo sahihi ukisema utoroshaji umefanyika ili hali ni mgodi mmoja pekee wa Iraqw mining uliozalisha kwa wingi.

"Kuna uchimbaji na uzalishaji, hivyo hivi sasa ni kipindi cha uchimbaji na wameanza kuzalisha kwenye baadhi ya migodi hivyo mwezi wa nane kutakuwa na mapato mengi yatakayotokana na mrabaha utakaolipwa serikalini," amesema Mnyeti.

Chanzo: mwananchi.co.tz