Dar es Salaam. Mkuu wa Wilaya ya Chemba, Simon Odunga amefungua kesi mbili za madai ya talaka kwa wake zake wawili katika Mahakama ya Mwanzo ya Ukonga.
Katika kesi moja ya kesi hizo ambayo ni ya madai namba 180 ya 2019, iliyo mbele ya Hakimu Elia Mrema, Odunga anaomba talaka dhidi ya ndoa ya Serikali aliyofunga Februari 21, 2010 na Ruth Osoro.
Pia, anaomba apewe ridhaa ya kumlea mtoto wao wa kiume wa miaka minne bila bughudha yoyote.
Mbali na kesi hiyo dhidi ya Ruth ambayo itasikilizwa Agosti 19, Odunga pia atakuwa mahakamani hapo Julai 30 katika kesi nyingine ya mwaka 2019 dhidi ya ndoa aliyoifunga kanisani na mwanamke mwingine.
Katika kesi dhidi ya Ruth, Odunga anaomba kutoa talaka kwa mkewe huyo kwa sababu amechoshwa na ugomvi na kudhalilishwa sehemu zake za kazi ingawa aliieleza Mahakama kuwa hana shaka na malezi ya mama wa mtoto huyo ila anataka amlee mtoto wake ili aweze kuepuka kadhia ya kudhalilishwa kila mahali ikiwamo kazini.
Alidai kuwa wakati anamuoa alikuwa akitambua kwamba ana mwanamke mwingine lakini alikuwa hajafunga naye ndoa na kwamba alimuoa kwa kuwa walikuwa na mgogoro wa kifamilia na Ruth aliridhia hilo.
Pia Soma
- Diamond atajwa mkutano mkuu wa NCCR-Mageuzi
- Kila mtu apanga ratiba yake La Liga
- Ujumbe wa Mbatia kwa Rais Magufuli huu hapa
- Magufuli kuelekeza nguvu Tazara, atoa maagizo wizara ya fedha
Kwa upande wake Ruth, alipinga kutolewa kwa talaka akisema bado anampenda mumewe na anataka mtoto wake alelewe na wazazi wote.
Hata hivyo, aliiambia mahakama kuwa licha ya manyanyaso aliyopitia kutoka kwa mumewe huyo, kutelekezwa na mwanaye kwa miaka mitatu bila ya kupewa matumizi, amemsamehe.
Kwa habari zaidi soma gazeti la Mwananchi la leo Jumamosi Julai 27, 2019