Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Dkt Francis Michael amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Farida Mgomi kuhakikisha anamrudisha shule mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Sekondari ya Wasichana Ileje, aliyeacha shule kwa kisingizio cha wazazi kukosa mchango wa chakula na kwenda kufanya kazi za ndani katika mji wa Tunduma.
Mkuu wa Mkoa wa Songwe, Dkt Francis Michael amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Ileje, Farida Mgomi kuhakikisha anamrudisha shule mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Sekondari ya Wasichana Ileje, aliyeacha shule kwa kisingizio cha wazazi kukosa mchango wa chakula na kwenda kufanya kazi za ndani katika mji wa Tunduma. Awali mkuu wa shule hiyo, Sharon Kadinde alisema shule hiyo iliyoanzishwa mwaka 2023 ikiwa na wanafunzi 75 wa kidato cha kwanza, mwanafunzi mmoja alishindwa kuendelea na masomo kwa madai wazazi hawana uwezo wa kuchangia chakula shuleni hapo huku wengine watatu wakihamishwa.