Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mkurugenzi wa Rombo ‘kiboko’

73768 Rombo+pic

Mon, 2 Sep 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Moshi. Agizo la Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC), la kutaka mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Rombo, Margareth John awajibishwe, linaingia katika orodha ya kauli kali za viongozi dhidi ya utumishi wake.

LAAC imeingia katika orodha hiyo ya kuonyesha shaka dhidi ya utendaji wake baada ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na katibu mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally pia kuonyesha wasiwasi naye.

Alipotafutwa kwa simu jana kuulizwa kuhusu ongezeko la kauli dhidi yake, Margareth alipokea na kusikiliza swali la mwandishi na alipoulizwa anazungumziaje maagizo hayo ya LAAC ya kuchukuliwa hatua za kinidhamu, alikata simu.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Tamisemi), Seleman Jafo pia hakupatikana kuzungumzia suala hilo na alipopigiwa simu, alirudisha ujumbe kuwa atafutwe baadae.

Juzi, mwenyekiti wa Kamati ya LAAC, Vedasto Ngombale aliagiza mamlaka zinazohusika kumchukulia hatua za kinidhamu DED huyo kwa kushindwa kumudu nafasi yake.

Kamati hiyo pia iliagiza kushitakiwa kwa watumishi wa wilaya hiyo waliotajwa katika ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kuhusika na ubadhirifu wa fedha.

Pia Soma

Advertisement   ?
Katika ukaguzi huo uliofanywa katika kipindi cha 2014/2015 hadi 2016/2017, watumishi wawili walianzisha mchakato wa malipo na kujilipa bila kufuata taratibu za malipo za Serikali.

“Ukifuatilia kama dokezo lilianzia kwa mkuu wa idara husika, huoni dokezo. Kwa hiyo kuna ujanja ujanja unafanyika mpaka watu wanajilipa,”alisema.

Kwa undani wa Habari hii pata nakala ya Gazeti la Mwananchi, Septemba 1, 2019

Chanzo: mwananchi.co.tz