Mwanamke mjamzito anayefahamika kwa jila la Anna Michael (47) mkazi wa kata ya Dumbeta wilaya ya Hanang mkoani Manyara, amekatika mguu wa kulia kiasi cha kutenganishwa na mwili wake, baada ya kukanyagwa mguu huo na tembo wakati akimuokoa mtoto wake asiuawe na kundi la tembo nje ya nyumba yake wilayani humo.
Anna akizungumza na waandishi wa habari akiwa katika Hosptali ya Rufaa ya mkoa wa Manyara, amesema tembo alimkanyaga mguu na ukakatika na kutengana na mwili hapo hapo eneo la tukio.
Aidha, Anna ameiomba Serikali imsaidie mguu wa bandia pamoja na mtaji wa biashara ili aweze kuacha kufanya kazi ya kupasua kokoto kutokana na hali yake ya sasa ya ulemavu. #GADITVUPDATES