Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Miundombinu Dodoma shaghalabaghala

56943 Pic+dodoma

Tue, 14 May 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dodoma. Meneja wa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura)Dodoma, Geoffrey Mkinga amesema ujenzi wa miundombinu unakabiliwa na changamoto ya ujenzi holela katika jiji hilo.

Akizungumza na Mwananchi kuhusiana na ujenzi wa mtandao wa barabara katika jiji la Dodoma jana, Mkinga alisema kwa sasa mtandao wa barabara hauko kwenye hali nzuri kutokana na halmashauri ya jiji kupima na kugawa viwanja bila kufungua barabara za maeneo hayo.

“Na ndiyo maana utakuta kuna makorongo yanayopitisha maji ya mvua lakini hakuna sehemu maalum ya kuyapeleka maji hayo na hata kama ukisema uyapeleke mahali fulani utajikuta umeyaelekeza kwenye nyumba ya mtu,” alisema.

Mkinga alisema wanachokifanya sasa ni kutafuta mhandisi msaidizi ili afanye usanifu kwenye makorongo yote yanayopitisha maji ya mvua na watakapoyatambua watayaombea bajeti kwa ajili ya kuyajenga na kusafirisha maji hayo.

“Jiji la Dodoma lina jumla ya kilomita 846 za barabara ambazo zimeshafunguliwa na zaidi ya kilomita 564 ambazo bado hazijafunguliwa na zipo kwenye makazi ya watu.”

“Hizo ni baadhi ya kilomita za barabara ambazo zinajulikana, lakini kuna zaidi ya kilomita 120 zinazojumlisha barabara za mzunguko pamoja na zile zilizopo katika mji wa Serikali,” alisema.

Pia Soma

Mapema wiki hii, mkurugenzi wa jiji la Dodoma, Godwin Kunambi alitia saini mkataba wa kukusanya na kuvuna maji ya mvua pamoja na uondoshwaji maji taka katika jiji hilo na mamlaka mbalimbalizinazohusika ikiwamo Tarura na Mamlaka ya Majisafi na Majitaka (Duwasa).

Chanzo: mwananchi.co.tz