Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Miradi mitatu Manispaa ya Kinondoni kuendelea

Ca804796339ae3a392125dfb171a86c1 Miradi mitatu Manispaa ya Kinondoni kuendelea

Sat, 30 Oct 2021 Chanzo: www.habarileo.co.tz

MKUU wa Mkoa wa Dar es salaam, Amos Makalla, ametembelea miradi mitatu ambayo ilielekezwa kusimama ujenzi wake na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Ummy Mwalimu, kutokana na kasoro zilizoonekana ambapo amesema muda wowote kuanzia sasa atatoa barua ya kuelekeza kuendelea kwa miradi hiyo

Miongoni mwa miradi hiyo ni Jengo la utalawa Manispaa ya Kinondoni linalogharimu sh Bilioni 2, Uwanja wa Timu ya KMC na Kituo cha Daladala cha Mwenge

Juni 20 mwaka huu, Ummy, alifikia uamuzi wa kusimamisha miradi hiyo baada ya kuikagua na kutoridhishwa na ujenzi wa miradi hiyo kwani tangu ilipoanza hadi alipotembelea Juni 20,2021 ilikuwa imefikia asilimia 46 ya utekelezaji wake, licha ya kuongezewa muda.

''Sijaridhishwa na hatua za ujenzi wa stendi ya mabasi Mwenge, zipo sarakasi kwenye huu mradi zipo sintofahamu kubwa ili niweze kujiridhisha nasimamaisha ujenzi na naunda timu ya kuchunguza miradi yote mitatu stendi ya Mwenge, uwanja wa mpira pamoja na jengo la utawala wa Manispaa ya Kinondoni nataka kujiridhisha,'' alisema Ummy, Juni 20, 2021

Pia aliunda timu huru ya kuchunguza mikataba yote ya miradi hiyo ili kujiridhisha, ikiwa ni pamoja na kumsimamisha kazi Mhandisi wa Manispaa Isack Mpaki

Hata hivyo, Makalla leo amesema kasoro zilizojitokeza zimerekebishwa na muda wowote kuanzia sasa atatoa barua ya kuelekeza kuendelea kwa miradi hiyo.

Aidha Makalla amewapongeza Manispaa ya Kinondoni kwa kutekeleza miradi mikubwa kwa mapato ya ndani.

Chanzo: www.habarileo.co.tz