Maandalizi ya kuaga miili ya marehemu 16 ikiwemo 14 wa familia moja waliofariki katika ajali usiku wa kumkia Februari 4, 2023.
Miili hiyo inaagwa katika viwanja vya Hospital ya Magunga, Korogwe kabla ya kusafirishwa kupelekwa mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya mazishi.
Katika ajali hiyo iliyotokea eneo la Magira Gereza, Tarafa ya Mombo, wilayani Korogwe, watu 17 walifariki dunia na wengine 12 kujeruhiwa.
Magari yaliyohusika katika ajali hiyo ni Mitsubish Fuso iliyogonga gari aina ya Coaster iliyokuwa imebeba mwili wa marehemu na abiria 26, ikitokea Dar es Salaam kuelekea Moshi Kilimanjaro kwa mazishi.