Miili ya wanafunzi watatu wa shule ya msingi Buhangija, iliyoko Manispaa ya Shinyanga waliopoteza maisha baada ya bweni walilokuwa wamelala kuteketea kwa moto, imeagwa leo Novemba 25, 2022, katika hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga na kukabidhiwa kwenye familia zao kwa ajili ya mazishi.
Watoto hao walipoteza maisha baada ya bweni walilokuwa wamelala kuteketea kwa moto usiku wa Novemba 23, ambapo Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Sophia Mjema ameongoza zoezi la kuaga miili ya wanafunzi hao.
Kwa upande wake mwakilishi wa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Shinyanga Charles Ngelela amesema wamesikitishwa na vifo vya watoto hao huku viongozi wa dini wakatoa neno la faraja kwa wafiwa.