Thu, 25 Mar 2021
Chanzo: globalpublishers.co.tz
Miili ya Wanafamilia Watano Waliiofariki Pamoja Yaagwa Kimara Dar March 25, 2021 by Global Publishers
MAJONZI na simanzi vimetawala leo Alhamisi, Machi 25, 2021, kwa waombolezaji wakati wakitoa heshima za mwisho kwa miili ya wanafamilia watano wa Kimara mkoani Dar es Salaam waliofariki pamoja.
Ndugu hao wanadaiwa kufariki Machi 21, 2021, katika Uwanja wa Uhuru kutokana na msongamano walipokwenda kuuaga mwili wa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.
Mbunge wa Kibamba (CCM), Mtemvu Issa amewasili kwenye msiba huo leo Alhamisi, kutoa pole kwa familia hiyo.
Chanzo: globalpublishers.co.tz