Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mifuko mbadala, vikapu vyatawala wilayani Temeke

60840 Pic+temeke

Mon, 3 Jun 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Katazo la matumizi ya mifuko ya plastiki limeonekana kuzingatiwa vyema na wakazi wa Wilaya ya Temeke, jijini Dar es Salaam.

Leo Jumamosi Juni Mosi, 2019 Mwananchi limezunguka  maeneo mbalimbali ya wilaya hiyo hasa yenye  wafanyabiashara wengi na kutoshuhudia mifuko ya plastiki.

Hata waliokuwa wakifika kwenye maeneo hayo kwa ajili ya kujipatia mahitaji mbalimbali walionekana wakiwa na mifuko mbadala.

Katika masoko ya Tandika na Stereo, wanawake wengi walionekana wakiwa wamebeba vikapu kwa ajili ya kuwekea mahitaji yao.

Mkazi wa Mtoni, Rehema Mbiku ameeleza kuwa katazo hilo limewarudisha wanawake nyakati za kubeba vikapu wanapokwenda sokoni.

“Kwa kiasi fulani linaturudisha enzi za mwanamke wa Kitanzania kwenda sokoni na kikapu binafsi naona Serikali imefanya kitu kizuri mifuko ilikuwa inachafua mazingira,” amesema Mbiku.

Pia Soma

Edson Temba, mmiliki wa duka katika soko hilo amesema jana usiku alilazimika kuchoma mifuko yote ya plastiki iliyokuwa dukani kwake ili kwenda sawa na agizo hilo.

Chanzo: mwananchi.co.tz