Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mgomo wa daladala Mbeya, nauli zapaa

47247 Pic+mbeya

Tue, 19 Mar 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Mbeya. Wananchi wa Jiji la Mbeya kwa mara nyingine wamekumbana na adha ya usafiri kukufuatia mgomo wa daladala ulioanza mapema leo asubuhi Jumatatu Machi 18, 2019.

Baadhi ya wananchi wamesema mgomo huo umewaathiri kutokana na nauli kupanda kutoka Sh500 kwa pikipiki za magurudumu matatu (Bajaj) na kuwa Sh1,000.

Hussein Juma amesema yeye anafanya biashara Mbalizi lakini amechelewa kutokana na kukosa usafiri na nauli kuwa juu.

"Mgomo umetuathiri sana badala ya kulipia Sh450 kwa daladala nalazimika kulipia Sh 1000," amesema.

Ibrahim Chaula ambaye ni msafiri pia amesema wameathirika kwa sababu mgomo huo umesababisha mambo yao kuchelewa na mengine kukwama kabisa.

Soma zaidi: Daladala Mbeya zagoma, abiria wasota

Related Content

Jacob Muhule mkazi wa Sae amesema mgomo umekuwa na changamoto nyingi na kuomba Serikali kutatua tatizo hili kwa haraka kwa kuwa linawakwamisha kimaendeleo.

Endelea kufuatilia Mwananchi kujua kinachojiri zaidi



Chanzo: mwananchi.co.tz