Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mghwira ampa saa 48 mwekezaji kujisalimisha

17480 Mgwira+pic TanzaniaWeb

Mon, 17 Sep 2018 Chanzo: mwananchi.co.tz

Hai. Mkuu  wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira ametoa  saa 48 kwa msimamizi wa mashamba ya Kahawa ya Kibo na Kifaru,Trevo  Giffod Wilayani Hai kujisalimisha mikononi mwa Polisi.

 

Mghwira ametoa agizo  hilo leo Septemba 15 baada ya  Giffod kukimbia kikao alichokiitisha Mkuu huyo  kutokana na uwepo wa utata wa mwekezaji  halali wa mashamba hayo.

 

Giffod anadaiwa kutoroka kikao alichoitisha Mghwira baada ya kukubaliana kukutana naye ili kujadili kuhusu utata wa uwekezaji wa shamba hilo.

 

Akizungumza na kamati ya ulinzi ya wilaya pamoja na wafanyakazi wa mashamba hayo Mghwira alisema kama mashamba hayo yanamilikiwa kihalali  na Giffod, iweje akimbie mkutano huo?

 

Mmiliki halali wa mashamba hayo ni  vyama vinne vya msingi vya ushirika ikiwamo Masama Roo, Masama Sawe, Sonu Ngira na Mudio (Mrososangi) ambavyo viliingia mkataba na mwekezaji Konrald Legg mwaka 1999.

 

Baada ya Legg kushindwa kuliendesha alimpa mwekezaji mwingine, ambaye ni Giffod, kinyume na mkataba.

 

Sambamba na mmiliki huyo kujisalimisha Polisi, Mghwira alimtaka Mkuu wa Wilaya ya Hai, Lengai Ole Sabaya kumpa taarifa halisi za nani mmiliki wa mashamba hayo.

"DC naomba nipate taarifa sahihi za nani mmiliki wa shamba hili mapema kwa sababu mmiliki huyu wa Sasa alikana kampuni hizi sio zake,hatukubali  kuendeshwa Kama gari bovu nataka nione vyama hivi vya ushirika vinaona faida yake,"amesema Mghwira

 

Hata hivyo, uongozi wa ushirika unaomiliki  mashamba  hayo umedai kuwa wao wanamtambua mwekezaji Konrald Legg  ambaye ni raia wa Ujerumani waliyeingia  naye mkataba tangu mwaka 1999 hadi mwaka 2029 kwa kipindi cha miaka 30 ili kuendeleza kilimo cha kahawa wilayani humo.

Katibu wa mashamba hayo, Jubilathe Ndossi alikiri kuwa wanamtambua mwekezaji wa kwanza waliyeingia naye mkataba wa miaka 30 kwa ajili ya kuendeleza kilimo cha kahawa.

Maliki Lema ambaye ni kibarua katika mashamba hayo amesema kuwa wao kama vibarua hawajui chochote kuhusiana na wamiliki wa mashamba hayo.

 

"Sisi hatuhitaji kuhoji uongozi wa mashamba haya,tunataka tupate stahiki zetu bila kubabaishwa pia hatuwezi kuhoji mabosi zetu," alisema Lema.

Chanzo: mwananchi.co.tz