Hata hivyo katika hali ambayo pengine hakuitarajia, alikuta mlango wa ofisi yake umebadilishwa nywila ya kuingilia hali iliyomlazimu kusubiri nje ya ofisi hiyo.
Akizungumza na MCL, Mwita amesema kufuatia hali hiyo hawezi kuingia ndani mpaka atakapojiridhisha.
Katika hali ya kushangaza walinzi waliokuwepo eneo hilo walikuwa wakizuia mtu yeyote kuingia katika ukumbi huo kwa maelekezo kuwa mpaka wapate kibali kutoka juu.
Pia wakati waandishi wakiondoka eneo hilo walimshuhudia diwani wa Tabata, Patrick Asenga naye akizuiwa kuingia.
Kwa Taarifa Zaidi endelea kusoma Mwananchi na kufuatilia mitandao yetu