Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mbunge, diwani watofautiana ujenzi kituo cha afya

Mbungeeepic Data Mbunge, diwani watofautiana ujenzi kituo cha afya

Sun, 12 Dec 2021 Chanzo: www.mwananchi.co.tz

Mvutano wa kugombea eneo la kujenga kituo cha afya kati ya kijiji cha Njinjo na Kipindimbi wilayani Kilwa Mkoa wa Lindi umechukua sura mpya baada ya mbunge wa Kilwa Kusini, Francis Ndulane na diwani wa Njinjo, Nurudini Abdallah kurushiana maneno.

Abdallah amesema alipigiwa simu na mbunge huyo akitaka kujua msimamo wake kuhusu ujenzi wa eneo hilo na kumjibu kuwa ni Njinjo akisisitiza kuwa ni msimamo wa kikao cha kamati ya maendeleo ya kata.

"Baada ya majibu  hayo mbunge  alisema kama ndiyo wanatofautiana wenyewe kwa wenyewe basi  ataona kama mwaka 2025  atashinda udiwani kwamba atahakikisha  uchaguzi ujao sipati ushindi."

"Mimi nilichaguliwa na wananchi na yeye   alichaguliwa na  tusubiri uchaguzi ujao utaeleza," amesema.

Kwa upande wake Ndulane amesema ujenzi wa kituo hauna mjadala utafanyika  kijiji cha Kipindimbi na  tayari barua ya maelekezo kutoka wizarani imeletwa inayobadili ujenzi wa kituo hicho kutoka kijiji cha Njinjo kwenda  kijiji cha  Kipindimbi .

"Mimi kwa sasa sina muda wakuongelea haya mambo nimebanwa nina mambo mengine naenda kushughulikia hoja za wananchi kata ya  Somanga, nimepanga siku rasmi kuzungumzia mambo hayo, nitafanya kikao na waandishi wa habari mkoani," amesema Ndulane.

Advertisement Musa Mohamedi mkazi wa Kipindimbi amesema kitendo cha viongozi kutofautiana kwenye suala lenye maelekezo ya Serikali linaweza  kuwagawa wananchi.

Chanzo: www.mwananchi.co.tz