Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Dunstan Kitandula amesema Serikali imeunda Kamati ya Kitaifa ya kuratibu namna bora ya kurudisha nchini na kunufaika na malikale zilizopo nje kikiwemo Kimondo cha Ivuna.
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii Dunstan Kitandula amesema Serikali imeunda Kamati ya Kitaifa ya kuratibu namna bora ya kurudisha nchini na kunufaika na malikale zilizopo nje kikiwemo Kimondo cha Ivuna. Kitandula ametoa kauli hiyo bungeni jijini Dodoma kufuatia swali la Mbunge wa Momba, Condester Sichalwe aliyetaka kufahamu ni lini Serikali itakirejesha nchini Kimondo cha Ivuna kilichopelekwa nchini Uingereza miaka zaidi ya 80 iliyopita ili kitumike kama kivutio cha utalii hapa nchini.