Mon, 13 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Waziri wa Ujenzi, Inncont Bashungwa, Waziri wa TAMISEMI, Mohamedi Mchengerwa na RC wa Dar es salaam Albert Chalamila wamefika eneo la Jangwani Jijini Dar es salaam muda huu ili kuona hali ilivyo katika eneo hilo.
Itakumbukwa jana barabara ilifungwa kwa muda eneo la Jangwani kutokana na kutopitika kufuatia uwepo wa maji mengi barabarani baada ya mvua kubwa kunyesha, ingawa leo barabara inapitika kama kawaida.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live