Fri, 14 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mmiliki wa kampuni ya Tunakodisha Furniture ambayo inamiliki maduka yaliyoteketea kwa moto katika eneo la Amani Zanzibar Bwana Khamis Juma amesema zaidi ya shilingi milioni Mia Mbili zinakadiriwa kupotea kufutia kuungua moto kwa Samani (Furniture) katika maduka yake yaliyopo Amani Zanzibar Ameeleza hayo wakati wa tukio la kuungua moto maduka yake majira ya saa 3 asubuhi huko Amani Mjini Unguja
Amesema thamani pekee za Furniture hizo ni Shilingi Milioni Mia Mbili huku kukiwa kuna fedha taslim shilingi Milioni Mbili pamoja na thamani ya maduka yaliyopo katika eneo hilo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live