Hai. Mamia ya watu wamejitokeza katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Nshara Machame kushiriki misa ya mazishi ya Meja Jenerali mstaafu, Alfred Mbowe.
Alfred Mbowe alifariki dunia Jumapili Julai 28, 2019 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, aliagwa jijini Dar es Salaam Jumatano Julai 31, 2019 na kusafirishwa kwa ajili ya mazishi yanayofanyika leo.
Mazishi ya Alfred ambaye ni kaka wa mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe yatafanyika katika kijiji cha Nshara Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro.
Viongozi mbalimbali wamefika katika kanisa hilo kushiriki misa hiyo itakayoanza saa 7 mchana.
Alizaliwa Januari 1953 na kujiunga na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) mwaka 1973 na kustaafu utumishi jeshini mwaka 2009, akiwa amelitumia jeshi hilo miaka 36.