Dar es Salaam. Mamia ya watu wamejitokeza katika Kanisa Katoliki Tabata Kinyerezi jijini Dar es Salaam kuaga mwili wa aliyekuwa ofisa mwandamizi Wizara ya Fedha na Mipango, Leopold Lwajabe.
Lwajabe aliyekuwa mkurugenzi wa miradi inayotekelezwa na Umoja wa Ulaya nchini (EU) kupitia wizara hiyo, mwili wake ulikutwa wilayani Mkuranga mkoani Pwani Julai 26, 2019 ukining’inia juu ya mti wa mwembe kwa mujibu wa familia yake.
Misa ya kuaga mwili wa Lwajabe imefanyika leo mchana Agosti Mosi, 2019 na kuhudhuriwa na watu wa kada mbalimbali, wakiwemo mabalozi.
Mwili wa Lwajabe unatarajiwa kusafirishwa leo kuelekea Ihembe, Karagwe mkoani Kagera kwa mazishi yatakayofanyika Agosti 3, 2019.