Dar es Salaam. Mama mzazi wa mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ Desderia Mbilinyi amefariki dunia leo Jumapili Agosti 26, 2018 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Taarifa iliyotolewa leo na uongozi wa Muhimbili imesema, Desderia alikuwa amelazwa hospitalini hapo na hali yake ilibadilika usiku wa kuamkia leo na kuhamishiwa chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU).
“Mama mzazi wa Sugu (Mbunge) amefariki leo saa 3:00 asubuhi (akiwa) ICU,” imeeleza taarifa ya Muhimbili na kuongeza kuwa mwili umehifadhiwa hospitalini hapo.
Soma zaidi:Sugu asema afya ya mama yake itaamua lini ataibuka bungeni