Fri, 10 Feb 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Diana Joseph Mkazi wa Tabata Kimanga Dar es Salaama na mtu mwingine mmoja ambaye jina lake halijafahamika wanashikiliwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumuua msichana wa kazi za ndani.
Mwanamke huyo anayetuhumiwa kufanya tukio hilo usiku wa kuamkia leo inadaiwa amekuwa na mfululizo wa matukio ya ukatili kwa wasichana wake wa kazi kwa kuwapiga na kuwachoma na pasi.
Si hayo tu, inadaiwa pia amekuwa akiwafanyia ukatili huo wajukuu zake ambao wamelazimika kukimbilia kwa wazazi wao.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live