Mon, 19 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Jeshi la polisi Mkoani Mtwara linamshiklia mwanamke mmoja mkazi wa Kijiji cha Sinde Kata ya Msangamkuu, halmashauri ya Mtwara, kwa tuhuma za kumnyonga mtoto wake mwenye umri wa miaka miwili na nusu.
Baadhi ya majirani wanasema mama huyo alimnyonga mtoto wake huku yeye na mtoto wakiwa uchi na kukimbilia porini ndio majirani walipomkimbiza na kumchukua mtoto lakini alikuwa tayari amefariki.
Kaimu Kamanda jeshi la polisi Mkoa wa Mtwara, ACP Nicodemus Katembo amesema mtuhumiwa atafikishwa mahakamani pindi uchunguzi utakapokamilika.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live