Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara linamshikilia Mwananzige Dadi (34) mkazi wa Kijiji cha Sinde, Kata ya Msangamkuu Kwa kosa la kumuua mtoto wake (4) kwa kumkaba.
Akizungumza na waandishi wa habari, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara, Nicodemus Katembo amesema kuwa Disemba 12, 2022 saa nne usiku katika Kitongoji cha Ngw'ale Kijiji cha Sinde Dadi almkaba shingo mtoto wake hadi kusababisha kifo.
Amesema kuwa baada ya uchunguzi wa kitabibu uliofanywa na daktari ilibainika kuwa chanzo cha kifo ni kukosa hewa baada ya kukabwa shingoni.
"Kwasababu tuko kwenye upelelezi ukikamilika mtuhumiwa atafikishwa mahakamani kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria," amesema.