Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mama Salma Kikwete atoa misaada kwa waathirika wa mafuriko Lindi

Mama Salma Kikwete atoa misaada kwa waathirika wa mafuriko Lindi

Mon, 3 Feb 2020 Chanzo: mwananchi.co.tz

Lindi. Mbunge wa kuteuliwa, Mama Salma Kikwete ametoa msaada  wa bati, chakula, mavazi, sabuni  pamoja na maturubai  kwa wahanga wa mafuriko mkoani Lindi.

Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya mama Salma leo Jumapili Februari 2, 2020, Katibu wa CCM Wilaya ya Lindi, Rukia Hassani  kwa Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Shaibu Ndemanga amesema  Mama Salma, ameguswa na tatizo lililotokea  hivyo ametoa msaada  wa vitu mbalimbali kwa waathirika hao.

Rukia  amesema  Mama Salma amejitolea kutoa msaada huo kwa jamii iliyokumbwa  na maafa hayo  baada ya kutembelea baadhi ya maeneo yaliyokumbwa na mafuriko ya Lindi vijijini, Kitomanga na Nangaru.

 Amesema  juhudi za makusudi zinahitajika  kuchukuliwa kutokana na waathirika hao  kuhitaji misaada ya kijamii kama ya makazi chakula , mifugo na  mazao yao kusombwa na maji.

“Hatuna budi kutoa shukrani kwa msaada  wake kwani hii inaonyesha anajali wananchi  kwa moyo wa uzalendo,” amesema Rukia.

Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Ndemanga amesema  Mama Salma ameonyesha moyo wa  kuwathamini jamii yenye matatizo  na kujali janga la mafuriko ambalo limeathiri  kwa kiasi kikubwa shughuli za kimaendeleo na kuwaomba wadau wengine kuiga mfano huo.

Pia Soma

Advertisement
“Tunahitaji sana misaada vitu mbalimbali kama  ya chakula,  nguo, dawa, kwani mpaka sasa tuna kambi nne zenye watu zaidi 843 waliokumbwa na mafuriko Lindi vijijini,” amesema mkuu wa wilaya ya Lindi Shaibu Ndemanga.

Ndemanga  amesema pamoja na misaada inayotolewa serikali  imetenga maeneo ya  viwanja ambavyo vitagawiwa kwa wananchi wote waliokumbwa na mafuriko ili wakaendelee na shughuli zao za kuwaletea maendeleo.

Chanzo: mwananchi.co.tz