Sat, 4 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ajali mbaya imetokea baada ya lori lenye namba za usajili T 447 DVV kugongana uso kwa uso na lori lenye namba za usajili T 233 DSS.
Ajali hiyo imetokea alfajiri ya leo Jumamosi, Machi 4, 2023 katika eneo la Stendi mpya Chalinze mkoani Pwani.
Tqarifa za awali zineleza kuwa, dereva wa lori namba T 447 DVV amevunjika mguu na amekimbizwa hospitali ya Chalinze.
Mashuhuda wa ajali hiyo wanasema madereva wa malori yote walikuwa wanakwepa gari bovu ambalo lilikuwa limeegeshwa pembeni mwa barabara.
Taarifa zaidi tutakujuza.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live