Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Makongoro Nyerere apokea Mwenge wa Uhuru Manyara

F718220d B3cc 4f11 8a84 74d4b9ffeff7 640x400.jpeg Makongoro Nyerere apokea Mwenge wa Uhuru Manyara

Sat, 12 Jun 2021 Chanzo: millardayo.com

Mwenge wa uhuru umeingia Mkoani Manyara ukitokea Kilimanjaro na unatarajia kukagua, kutembelea, kuona na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi 29 yenye thamani ya sh6.6 Bilioni.

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Charles Makongoro Nyerere, akizungumza mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro, wakati akipokea mwenge wa uhuru kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Stephen Kagaigai, amesema Mwenge wa Uhuru utakimbizwa kwa Kilomita 1,089.3.

Makongoro amesema Mwenge huo utaweka mawe ya msingi ya miradi 10 ya thamani ya sh3.7 Bilioni na kuzindua miradi minne ya thamani ya sh342.3 milioni.

Amesema utafungua miradi mitatu ya thamani ya sh534.3 milioni na kukagua na kuona miradi 12 ya thamani ya sh2 bilioni.

“Mwenge wa uhuru utakimbizwa kwenye tano za Simanjiro, Kiteto, Babati, Hanang’ na Mbulu, kisha kuukabidhi mkoa wa Arusha Juni 16,” Makongoro.

WANAFUNZI WAJENGEWA UWEZO KUFANYA MAAMUZI, KUJIEPUKA NA VISHAWISHI KIPINDI CHA LIKIZO

Chanzo: millardayo.com