Dar es Salaam. Unaweza kusema kauli aliyoitoa mbunge wa Kibamba (Chadema), John Mnyika katika hafla ya uwekaji jiwe la msingi la upanuzi wa barabara ya Morogoro jijini Dar es Salaam iliyofanyika eneo la Kimara Stop Over imemshangaza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.
Kauli hiyo ya Mnyika imemfanya Makonda kuwashangaa wabunge wa upinzani wanaokosoa jitihada zinazofanywa na Rais John Magufuli.
Makonda ameyaeleza hayo leo Jumatano Desemba 19, 2018 katika hafla hiyo baada ya Mnyika aliyepewa nafasi ya kusalimu wananchi na kugusia suala la demokrasia, kutaka waliobomolewa nyumba kupisha upanuzi huo kulipwa fidia na kudai kuwa wananchi mtaani vyuma vimekaza.
Baada ya Mnyika kumaliza kuzungumza, Makonda amesema anashangazwa na mbunge huyo kutaka wananchi walipwe fidia badala ya kusifia mradi huo.
Amesema licha ya jitihada zinazofanywa na Rais Magufuli bado kuna watu wanampinga, huku akitolea mfano elimu bila malipo na ununuzi wa ndege.
“Mnamhukumu kuwapatia fedha, mnamhukumu kwa kupanua barabara nane ili msipate tabu ya usafiri. Hivi mnapokaa nyie na akili zenu mnawaza nini, na mbaya zaidi hata ofisi zao pale makao makuu wameshindwa
kuzitengeneza,” amesema Makonda.